MBS logo 12 kb   

Missionary Benedictine Sisters

Peramiho, TANZANIA, East Africa

Home | Location | History | Education | Health Care | Orphanages | Out Stations  | Music  | Contact

Nyumbani | Mahali Maalum | Historia | Schule | Afya | Yatima | Out Stations | Musik CD | Mgusano & Msaada

Historia Kifupi ya PeramihoSrs. Odilia & Gloria
                              Sehemu ya III

   <-Historia I    <- Historia II

Mabadiliko na Nyakati wa Siku Hizi

1971-1976   Uongozi ulikuwa mikononi mwa Sr. M Elizabeth Sarinas OSB toka Ufilipino. Kwa mara ya kwanza masista kutoka Ufilipino walikuja kusaidia Priorati ya Peramiho.

1976-1987    Kiongozi wa Jumuia ya Peramiho alikuwa Sr. M. Isentrud Lehner. Inakumbukwa kuwa wakati huu wasichana Waafrika walianza kualikwa kujiunga na shirika la Wamisionari Wabenediktini wa Tutzing ili kuendeleza kazi ya Umisionari kama Baba Benedikto anavyosisitiza (Sala na kazi ).

Wasichana waliojiunga Peramiho walitakiwa kwenda Nairobi kupata malezi yao kuanzia mwaka 1982 hadi 1995. Mwaka 1996 malezi yalifanyika hapa Tanzania.

Kuanzia mwaka 1962 idadi ya masista imepungua hatua kwa hatua. Mwaka 1990 jumuia ilikuwa na masista 44. Kwa hiyo, masista walioishi katika vituo vya maparokiani katika majimbo ya Songea, Mbinga na Njombe walirudishwa katika makao ya priorati Peramiho, iliyokuwa awali ya majimbo 3. 

Utamadunisho wa Shirika

Mwaka 1982 Mwafrika wa kwanza Mtanzania, leo Sr. M. Getrud Luoga wa Parokia Luwana Njombe, alijiunga na shirika la Masista Wamisionari Wabenediktini wa Tutzing Peramiho jambo ambalo lilileta sura mpya katika jumuia.   

Malezi ya watawa watarajiwa ya wakati ule kule Nairobi, yalijumuisha wasichana kutoka nchi za kiafrika. Wakati ule wasichana waliokuwepo walitoka Kenya, Uganda, Nigeria, Angola na Tanzania.

Malezi ya hapa Tanzania Peramiho yalitoa tunda la kwanza tarehe 10 Februari 1996 pale Sr. M. Gloria Haule wa Jimbo Kuu la Songea na Sr. M. Odilia Kipanga wa Jimbo la Morogoro walipoweka Nadhiri za Kwanza katika Kanisa la Abasia. 

Sasa malezi kwa ajili ya Priorati za Peramiho na Ndanda hufanyika hapa Peramiho. 

Wamama Wakubwa katika Wakati Huu
1963-1971  Sr. Verediana Wolfsteiner, OSB
1971-1976 Sr. Elizabeth Sarinas, OSB
1976-1987 Sr. Isentrud Lehner, OSB
1987-1995 Sr. Maria Goretti Gast, OSB
1995-2007 Sr. Pia Portmann, OSB
2007-Present Sr. Rosann Ocken, OSB