Hospitali ya Mtakatifu Yosefu Peramiho

1901

Masista 4 Wamisionari Wabenediktini miongoni mwao mmoja akiwa nesi na wengine wasaidizi wa Uuguzi waliwasili Peramiho. Kundi hili la masista lilitoa huduma ya kuwatunza   wagonjwa wa vijijini. Aidha waliwatunza wakoma wa kituo kilichokuwa karibu na eneo la Lundusi Peramiho.



Sr. Laurentia in old times


Sr. Twertigis in Nursing School


Entrance Peramiho Hospital


Sr. Fromunda with Leprose Patients


Br. Dr. Ansgar Stuefe

1909

Baada ya kuondoka Peramiho kwa sababu ya Vita vya Maji Maji, Masista walirudi Peramiho na wakaanza upya kufanya kazi zao. Nyakati zile wagonjwa walitibiwa Peramiho katika jengo la zahanati lililoezekwa nyasi. Wagonjwa wengine walitembelewa na kuhudumiwa kwenye makazi yao vijijini.

1911

Serikali ilijenga nyumba katika eneo la Morogoro kwa ajili ya kuishi wagonjwa wa ukoma na ikawakabidhi masista wahudumu jengo hilo.

1923

Kufukuzwa Wamisionari Wajerumani nje ya Tanganyika mwaka 1916 kulihitimisha kipindi cha kazi ya kimisionari kilichotangulia na kufungua kipya. Ili kuboresha huduma za afya, zilijengwa wodi za udongo kwa ajili ya kulala   wagonjwa. Kulitolewa mafunzo ya uuguzi kwa masista na wanakijiji kwa ajili ya huduma ya kituo cha afya. Dispensari zingine zilianzishwa katika maeneo ya Ungoni na Umatengo. Waganga wa hospitali ya wilaya ya Songea waliisaidia dispensari ya Peramiho kwa kutibu wagonjwa na kutoa ushauri.

1949

Hospitali Peramiho ilimpata Daktari Sr. M. Tetwigis Sailer OSB na hapo ikatunukiwa hadhi ya kuwa Hospitali.   Madaktari masista wengine waliongezwa; Sr. Maria Salus Linde OSB, Sr. Wernfried Walter OSB, Sr. Birgitta Schnell OSB.
Mwaka 1952 Daktari Sr. Tetwigis, alianzisha Chuo cha Uuguzi hapo hapo Peramiho kwa ajili ya Mafunzo ya Uuguzi na Ukunga kwa muda wa miaka 4.
Mwaka 1950 wodi ndogo ya kuta za udongo ya kulala wagonjwa wa kifua kikuu ilijengwa na matibabu yalianza mara moja. Baadaye iliboreshwa kwa kuta za matofali.
Hatua iliyofuata ilikuwa kuongeza majengo kwa ajili ya upasuaji, madawa, maabara na mwali-X au eksirei.

1980 - 2000

Ni kipindi cha mabadiliko makuu anuai: ujenzi wa majengo mapya, ukarabati wa majengo, ongezeko la idadi ya wagonjwa na madaktari bingwa, na uboreshaji wa tiba. Katika kipindi hicho hospitali ilikuwa na vitanda 420 na iliongozwa na daktari Br. Ansgar Stuefe OSB. Hospitali ilijiendeshea yenyewe Chuo cha Wauguzi na Ukunga ambacho kiliweza kupokea wanafunzi kuanzia 100 hadi 120. Awali wahitimu baada ya kozi ya miaka 4 walijipatia shahada. Toka mwaka 2004 wanachuo wakihitimu kozi yao walijipatia cheti cha Diploma au Stashahada. Tena kulitolewa mafunzo ya Wasaidizi wa Maabara kwa muda wa miaka 2. Wahitimu hutunukiwa Shahada la Wahudumu Wasaidizi wa Maabara.

Wakoma

Masista wetu walianza kukiendesha kituo na kuwahudumia wakoma tangu mwaka 1911 hadi sasa. Ufanisi wa huduma kwa kutoa dawa nzuri umefanikisha kutatua na kuponya shida mpya zilizojitokeza na idadi ya wagonjwa inapungua siku hadi siku isipokuwa shida za ulemavu wa shida za muda mrefu.

Mintarafu Ukimwi, kumejitokeza changamoto la watoto yatima. Kwa hiyo sista mhudumu wa kituo amelazimika kufungua kituo cha Watoto Yatima ambao sasa wamefikia idadi takriban 120. Watoto hutunzwa kuanzia umri wa mtoto mchanga hadi wanapofikia umri wa kupata ajira. Kumlea kila mtoto kadiri ya mahitaji yake ni changamoto zito linaloshinikiza shirika letu hususan suala la gharama. 

 

 

2003

Daktari Asngar Stuefe OSB aliondoka Peramiho na akahamia Ujerumani ambako alikabidhiwa wajibu mwingine katika shirika lake la Wamisionari Wabenediktini. Madaraka ya uongozi aliyakabidhi kwa Daktari Lemuel Rugumyamheto kama Naibu Mkurugenzi Mganga Mkuu na Daktari Venance Mushi kama Mganga Mkuu.