Historia ya Priorati ya Peramiho
1901 |
Tarehe 1 Julai Masista 4 wa Shirika la Wamisionari Wabenediktini wa Tutzing Sr. M. Constantia Mayr OSB, Sr.M. Valeria Kuhlman OSB, Sr. M. Mechtildis Dickhoff OSB na Sr. M. Magdalena Hessing OSB waliwasili Peramiho. Hapo nyumba ya masista wa Mtakatifu Sholastika ilianzishwa Peramiho. | ![]() Sr. Constatia, Sr. Valeria |
1905 |
Wakati wa vita vya Maji Maji vituo vya wamisionari vya kusini mwa Tanganyika viliathiriwa. Wapiganaji wa vita vya Maji Maji waliiharibu misioni ya Nyangao tarehe 29 Agosti na Peramiho mwezi Septemba na masista iliwapasa kutoroka. Tarehe 14 Agosti, wakiwa njiani kutoka Kilwa kuelekea Peramiho, Askofu Cassian Spiss, mabruda 2 na masisista M. Felicitas Hiltner na M. Cordula Ebert, waliuawa katika eneo la Liwale.
|
![]() Sr. Mechitildis, Sr. Magdalena |
1909 |
Baada ya hali kuwa tulivu Masista walirudi Peramiho. Hapo walitoa huduma ya kutibu wagonjwa katika hospitali na walianzisha shule ya wasichana iliyofikia idadi ya wanafunzi 110. |
![]() |
1911 |
Serikali iliwakabidhi masista eneo la Morogoro ambako walifungua kituo cha kutibu na kuwatunza wakoma. Huduma ilipoanza zahanati ilikuwa na wagonjwa takriban 200. |
|
1912 |
Viongozi wa Shirika kutoka Nyumba Kuu Ujerumani walizuru kituo cha Peramiho. Hapo walijionea yaliyotendeka na waliyarekodi hususan juu ya watu wengi waliobatizwa katika misioni husika, imani kubwa ya watu kwa wamisionari, shughuli za masista za kutunza wagonjwa, kufundisha watoto shuleni, kuwaendeleza zaidi kimasomo na na kadhalika. | |
1916
|
Vita Vikuu vya I vya Dunia vilisababisha masista waondoke tena nchini na kwenda Afrika ya Kusini. Mwaka 1920 masista walianzisha huko nyumba yao mpya. |
|
1923 |
Masista Wabenediktini wasio wa taifa la Kijerumani waliwasili Peramiho kuendeleza kazi ya kimisionari iliyoachwa wazi na masista walioondoka. Wakati huo huo wasichana wenyeji waliopenda kuishi maisha ya kimonaki walianza kupata malezi yaliyotolewa na masista wamisionari. Mwaka 1938, baada ya kukua, Shirika la Watawa Wabenediktini wenyeji wa Mtakatifu Agnes lilianzisha makao yake mapya huko Chipole. |
|
1926 |
Masista Wajerumani waliruhusiwa tena kuingia nchini kuendeleza huduma yao ya kimisionari. Shirika lilikua kwa kasi chini ya uongozi wa Abate Gallus aliyekuwa Kiongozi wa wakati ule. Masista walianzisha Chuo cha Ualimu, Chuo cha Ufundi fani ya Ushonaji na waliviendesha vyuo hivyo hadi pale mapadre na mabruda walipochukua nafasi ya kuviongoza na kuviendesha. Masista waliwafundisha waseminari wa kwanza somo la Kiingereza. Wakati wa kipindi cha uongozi wa Mama Priori M. Ermenilde Morrisey aliyesimikwa tarehe 26 Juni 1926, sister mmoja alikuwa mwalimu Mkuu wa shule ya msingi na mwingine aliongoza shule ya wasichana. Wakati Sr. M. Ermenilde akiwa madarakani na Priorati ikiwa na masista takriban 60, zilifunguliwa nyumba 13 katika Parokia mbali mbali. |
|
1934
to 1939 |
Sr M. Agata Ross OSB aliongoza jumuia ya Mtakatifu Sholastika Peramiho. | ![]() |
1939
- 1947 |
Uongozi ulikuwa mikononi mwa Sr. M. Kunigunde Weber OSB akiwa kiongozi wa tatu. | |
1947
- 1956 |
Sister M. Teodosia Biselli OSB alishika usukani. | |
1956
- 1963 |
Sr. M. Paula Knoepfle OSB alichaguliwa kuwa kiongozi wa jumuia. | ![]() |
1963
- 1971 |
Jumuia ilikuwa chini ya Sr. M. Verediana Wolfsteiner OSB | ![]() left: Sr. Verediana, Sr. Elizabeth, M. Gertrud |
1971
-1976 |
Uongozi ulikuwa mikononi mwa Sr. M Elizabeth Sarinas OSB toka Ufilipino. Kwa mara ya kwanza masista kutoka Ufilipino walikuja kusaidia Priorati ya Peramiho. |
|
1976
-1987 |
Kiongozi wa
Jumuia ya Peramiho alikuwa Sr. M. Isentrud Lehner. Inakumbukwa kuwa wakati
huu wasichana Waafrika walianza kualikwa kujiunga na shirika la Wamisionari
Wabenediktini wa Tutzing ili kuendeleza kazi ya Umisionari kama Baba Benedikto
anavyosisitiza ( Ora et labora yaani Sala na
kazi ) na kukabili upungufu wa miito ya masista wamisionari toka
Ulaya. |
![]() Sr. Isentrud, Sr. Heimrada, Sr. M.Goretti, Sr. Elisabeth, Sr. Verediana |
1987
- 1995 |
Priori wa Jumuia alikuwa Sr. M Goretti Gast OSB. | |
1995
- |
Sr. M. Pia Portmann ni Priori wa jumuia yetu ya Peramiho |
|
Kuanzia mwaka
1962 idadi ya masista imepungua hatua kwa hatua. Mwaka 1990 jumuia ilikuwa
na masista 44. Kwa hiyo, masista walioishi katika vituo vya maparokiani
katika majimbo ya Songea, Mbinga na Njombe walirudishwa katika makao ya
priorati Peramiho. |
||
Utamadunisho wa shirika Mwaka 1982 Mwafrika wa kwanza Mtanzania, leo Sr. M. Getrud Luoga wa Parokia Luwana Njombe, alijiunga na shirika la Masista Wamisionari Wabenediktini wa Tutzing Peramiho jambo ambalo lilileta sura mpya katika jumuia. Malezi ya watawa watarajiwa ya wakati ule kule Nairobi, yalijumuisha wasichana kutoka nchi za kiafrika. Wakati ule wasichana waliokuwepo walitoka Kenya, Uganda, Nigeria, Angola na Tanzania. Malezi ya hapa Tanzania Peramiho yalitoa tunda la kwanza tarehe 10 Februari 1996 pale Sr. M. Gloria Haule wa Jimbo Kuu la Songea na Sr. M. Odilia Kipanga wa Jimbo la Morogoro walipoweka Nadhiri za Kwanza katika Kanisa la Abasia. Sasa malezi kwa ajili ya Priorati za Peramiho na Ndanda hufanyika hapa Peramiho.
|
|
|